Home Makala Fainali Chan Kufanyika Nairobi

Fainali Chan Kufanyika Nairobi

by Dennis Msotwa
0 comments

Uwanja wa Taifa wa Kasarani uliopo jijini Nairobii nchini Kenya umechaguliwa kuwa uwanja utakaofanyika mchezo wa fainali wa Kombe la Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024, ambalo linafanyika nchini Kenya,Tanzania na Uganda.

Mchezo huo utachezwa Jumamosi Agosti 30, na unatarajiwa kuwa na mvuto kwa kiwango cha juu baada ya mashindano hayo ya  miezi miwili yanayotarajiwa kuvutia mashabiki wa soka katika nchi zote tatu za Afrika Mashariki.

banner

Kamati ya Maandalizi ya Local Organizing Committee (LOC) ilithibitisha kuwa uwanja huo, uliopo Nairobi, utakuwa ndio wa mwisho kwa michuano hiyo baada ya kukamilika kwa matengenezo yake.

“Tumalizika kwa uboreshaji wa Kasarani kunaleta fursa kwamba sasa tunaweza kutumia uwanja huo kwa mchezo wa fainali,” alisema Mwenyekiti wa LOC, Maurice Amollo.

Uwanja wa Kasarani pia utatumika kwa michezo mingine muhimu, ikiwa ni pamoja na mechi ya kufungua mashindano na nyingine za hatua ya makundi ambapo kundi A lenye timu za Kenya,Morocco,Angola,Dr Congo na Zambia.

Mechi nyingine za mashindano zitachezwa katika uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani, na uwanja wa Kinoru huko Meru.

Huu utakuwa mara ya kwanza Kenya kukumbwa na mashindano ya CHAN, ambayo ni ya timu za taifa zenye  wachezaji wanayocheza katika ligi za nyumbani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited