Home Makala Frank De Boer Apewa Mikoba Ya Koeman

Frank De Boer Apewa Mikoba Ya Koeman

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa Ajax,Frank De Boer ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uholanzi kwa ajili ya kujaza pengo lililoachwa na Ronald Koeman ambaye kwa sasa anainoa Barcelona baada ya Quique Setien kuvuliwa mikoba hiyo kutokana na matokeo duni.

De Boer ambaye pia aliwahi kuwa beki wa Ajax na Barcelona amepewa kandarasi ya miaka miwili kuitumikia timu hiyo ambao utatamatika mwishoni mwa fainali za kombe la Dunia zitakazoandaliwa nchini Qatar mwaka 2022.

Mchuano wa kwanza kwa De Boer kusimamia kambini mwa Uholanzi ni ule wa kirafiki utakaowakutanisha na Mexico jijini Amsterdam Octoba 7,2020 kabla ya kuwaongoza vijana wake kuvaana na Bosnia-Herzegovina na Italia katika UEFA Nations League Octoba 11 na 14 mwaka huu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited