Home Makala Gadiel Atua Singida All Stars

Gadiel Atua Singida All Stars

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Simba sc Gadiel Michael ambaye yupo katika orodha ya kutemwa klabuni hapo inasemekana tayari amefikia makubaliano ya kujiunga na timu ya Singida All Stars ambayo imepanda daraja kwenda ligi kuu msimu ujao.

Awali timu hiyo ilijulikana kama Dtb lakini hivi karibuni imebadilisha jina na kuitwa Singida All Stars huku ikiwa na mapango kabambe wa kushusha mastaa wa maana kwa ajili ya kuwasajili kwa msimu ujao wa ligi kuu na imeanza mazungumzo na mastaa hao akiwemo Gadiel ambaye hana namba katika kikosi cha Simba sc.

Mchezaji huyo anayecheza pembeni kushoto amekua na wakati mgumu tangu ajiunge na Simba sc akitokea Yanga sc akikosa namba mbele ya Mohamed Hussein na alikua katika hatihati ya kutemwa toka msimu uliopita wa ligi kuu na tayari inasemekana yupo katika orodha ya watakaotemwa msimu huu na klabu hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited