Home Makala Geita Gold Fc Wakumbwa na Rungu la Fifa

Geita Gold Fc Wakumbwa na Rungu la Fifa

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA limeifungia Klabu ya Geita Gold kutosajiri Mchezaji yeyote Mpaka pale itakapolipa Madai ya mishahara ya aliyekuwa Kocha wao Etienne Ndayiragije.

Geita Gold ilivunja mkataba na Ndayiragije baada ya kutoridhishwa na matokeo ya timu kwenye michezo yake ya awali mwanzoni wa Msimu huu na kuamua kumrejesha kocha Fred Felix Minziro ambaye aliipandisha timu hiyo daraja.

Kutokana na suala hilo inasemekana kwamba klabu hiyo haikukamilisha baadhi ya stahiki za kimkataba na kumfanya kocha huyo kukimbilia katika shirikisho hilo la soka duniani kudai haki zake na ndipo Fifa ilipojiridhisha imeamua kutoa hukumu hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited