Home Makala GSM yamkaribisha Manji kuwekeza Yanga

GSM yamkaribisha Manji kuwekeza Yanga

by Sports Leo
0 comments

Wadhamini wa klabu ya Yanga sc kampuni ya GSM imesema kuwa mwanachama na mwenyekiti wa zamani wa klanu hiyo Yusufu Manji yupo huru kununua hisa za timu hiyo.

Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa uwekezaji GSM Injinia Hersi alipokuwa katika mahojiano maalumu na kituo cha azam media.

Hersi alisema kuwa ”Manji anakaribishwa kununua hisa za klabu hiyo kwasababu mfumo wa umiliki wa hisa wa klabu ya Yanga si wa mtu mmoja, bali unaruhusu wawekezaji zaidi ya watatu”.

banner

Hilo limekuja mara baada ya kurejea kwa Manji kwenye mkutano mkuu wa mabadiliko wa klabu hiyo na kupelekea kushangiliwa kwa nguvu na wanachama wa Yanga hali iliyozua sintofahamu juu ya hatima ya GSM ambao wamekua mstari wa mbele kuipeleka Yanga kwenye mabadiliko.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited