Home Soka Guede Aondoka Singida Black Stars

Guede Aondoka Singida Black Stars

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Singida Black Stars Joseph Guede amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba wake na klabu hiyo kutokana na makubaliano ya pande zote.

Guede aliyesajiliwa klabuni hapo akitokea Yanga sc amefanikiwa kucheza mechi sita pekee za ligi kuu mpaka sasa ambapo hajafanikiwa kufunga bao lolote.

Uwepo wa washambuliaji Elvis Rupia,Athur Bada na Victorien Adebayo huku pia kiungo kama Marouf Tchakei ambaye anaweza kucheza kama mshambuliaji wa pili umeonekana kuwatosheleza mabosi wa Singida Black Stars kutohitaji tena huduma ya Guede.

banner

Guede baada ya kuvunja mkataba wake huo sasa anaangalia baadhi ya ofa alizonazo ndani ya bara la Afrika huku pia akihitajika na baadhi ya klabu za bara la Asia.

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini klabu hiyo imefikisha alama 30 ikiwa katika nafasi ya pili ya msimamo ikiwa imecheza michezo 14 ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited