Home Makala Hakuna Kupumzika Simba Waibuluza AFC 6-0

Hakuna Kupumzika Simba Waibuluza AFC 6-0

by Sports Leo
0 comments

Simba Sc leo imeibuka na ushindi wa mabao 6-0 mbele ya AFC leo kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Bao la kwanza na la tatu lilipachikwa na Meddie Kagere dakika ya 4 na 34 huku bao la pili lilifungwa na Larry Bwalya dakika ya 24.

Kipindi cha pili cha mchezo Simba Sc ilipachika mabao mengine matatu kupitia Luis Miqussone ambapo walifikisha idadi ya mabao 6-0 na kuwamaliza nguvu wapinzani  wa AFC.

banner

Simba wanajiandaa na mchezo wa ligi kuu bara dhidi ya Ihefu unaotarajiwa kuchezwa Septemba 6 uwanja wa Sokoine na AFC wao wanajiandaa na ligi daraja la kwanza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited