Home Makala Hapatoshi Yanga Sc Ikiwavaa Mc Algers

Hapatoshi Yanga Sc Ikiwavaa Mc Algers

by Sports Leo
0 comments

Jumamosi Januari 18 itakua siku maalumu kwa mashabiki wa Klabu ya Yanga Sc kutokana na timu hiyo kuwania tiketi ya kufuzu robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika itakapovaana na Mc Algers katika michezo ya mwisho ya kundi A la michuano hiyo.

Yanga sc ili ifuzu robo fainali lazima ipate alama tatu katika mchezo huo vinginevyo basi moja kwa moja itakua imetolewa katika michuano hiyo.

banner

 

Tayari klabu hiyo imeanza zoezi la kuuza tiketi za mchezo huo ambapo mpaka sasa mashabiki wameshaanza kuzinunua kwa wingi.

“Niwapongeze sana Mashabiki na Wanachama wa Klabu yetu kwa Kujitokeza mapema kununua tiketi za mchezo wetu dhidi ya MC Alger kabla ya kutangaziwa kwenye Mkutano na Wanahabari”,Alisema Ally Kamwe mkuu wa idara ya habari ya klabu ya Yanga sc.

“Niwapongeze mashabiki na wanachama wa Yanga Sc,Tiketi nyingi tayari zimeisha kabla hata mkutano wa hamasa au klabu kutangaza rasmi uuzwaji wa tiketi, mwamko wa Wanayanga umekuwa mkubwa sana,wananchi wameingia wenyewe kwenye mfumo wa N-Card na kununua tiketi bila klabu kutangaza chochote. Wananchi wameonesha kwa vitendo kwa kiasi gani wanaitaka mechi, VIP A tayar zimeisha”,Alimalizia kusema Kamwe

Yanga sc imeamua kushusha bei ya tiketi hizo ambapo kiingilio cha chini ni shilingi elfu tatu za kitanzania huku kiingilio cha juu ikiwa na shilingi elfu thelasini tu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited