Home Makala Ibrahimovic Atua Nchini

Ibrahimovic Atua Nchini

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa zamani wa Manchester United,Psg na Ac Milan Zlatan Ibrahimovic yupo nchini Tanzania kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatiakana hapa nchini.

Zlatan amechapisha picha kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram akiwa eneo la Kogatende kwenye hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini Tanzania eneo ambalo ni kitovu cha uhamaji wa wanyama maelfu wanaovuka Mto Mara kueleka nchini Kenya ama kuja nchini.

Inafahamika kwamba mwezi huu wa juni ndio msafara huo wa wanyama hasa nyumbu huvuka mto Mara kwa ajili ya kutafuta malisho tukio ambalo huwa ni la kiekolojia zaidi na huvutia watalii wengi duniani.

banner

Zlatan (43) raia wa Sweden ambaye amewahi pia kuichezea Ajax, PSG, AC Milan na Barcelona ambaye kwa sasa ni sehemu ya washauri wa klabu ya AC Milan yupo Tanzania kwa ajili ya mapumziko ya mwisho ya msimu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited