Home Makala Itakuwaje Salah Akikosekana Liverpool??

Itakuwaje Salah Akikosekana Liverpool??

by Dennis Msotwa
0 comments

Liverpool ni timu inayoongoza Ligi Kuu England kwa sasa ikiwa imecheza mechi 29 na kujikusanyia pointi 82,japo kwa sasa ipo kwenye hatihati ya kumkosa mshambuliaji wao Mohamed Salah raia wa Misri kwa muda wa miezi minne ya msimu ujao.

Jambo hili l inakuja kutokana na kuvurugika kwa ratiba za michuano mingi ya kimataifa kutokana na kuenea kwa virusi vya Corona ambapo michuano mingi ya kimataifa imebadili ratiba zao ikiwa ni pamoja na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Jurgen Klopp ambaye ni kocha mkuu wa Liverpool tayari ameanza kupasua Kichwa kujua ni nani atakayekuwa mbadala wa Salah iwapo mambo yatakuwa ndivyo sivyo.

banner

Kocha wa timu ya Taifa ya Misri chini ya miaka 23, Shawky Gharib amesema kuwa mchezaji Salah ana uwezo wa kipekee na kila kocha ambaye anafanya naye kazi ni lazima ampe nafasi ndani ya kikosi chake kutokana na uwezo aliokuwa nao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited