Klabu ya Azam Fc imekamilisha usajili wa kiungo mkabaji kutoka Rwanda ambaye alikuwa akicheza ndani ya Yanga Sc, Ally Niyonzima kwa mkataba wa miaka miwili.
Niyonzima aliyekuwa akicheza Rayon Sports Ya Rwanda pia yupo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Rwanda ‘Amavubi’, anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Azam FC kwa ajili ya msimu ujao huku usajili wa kwanza ni wa kiungo Awesu Awesu kutoka Kagera Sugar.
Usajili wake wa leo Agosti Mosi ni sehemu yamapendekezo ya benchi la ufundi la Azam FC chini ya Kocha Mkuu, Aristica Cioaba,pia amesini mkataba mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.