Home Makala Jembe La Yanga Atua Azam

Jembe La Yanga Atua Azam

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Azam Fc imekamilisha usajili wa kiungo mkabaji kutoka Rwanda ambaye alikuwa akicheza ndani ya Yanga Sc, Ally Niyonzima kwa mkataba wa miaka miwili.

Niyonzima aliyekuwa akicheza Rayon Sports Ya Rwanda pia yupo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Rwanda ‘Amavubi’, anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Azam FC kwa ajili ya msimu ujao huku usajili wa kwanza ni wa kiungo Awesu Awesu kutoka Kagera Sugar.

Usajili wake wa leo Agosti Mosi ni sehemu yamapendekezo ya benchi la ufundi la Azam FC chini ya Kocha Mkuu, Aristica Cioaba,pia amesini mkataba mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited