Home Makala Juventus Kumng’oa Mmoja Liverpool

Juventus Kumng’oa Mmoja Liverpool

by Sports Leo
0 comments

Taarifa inayosambaa kwa kasi ni kwamba Juventus imejipanga kumng’oa beki wa Liverpool Virgil van Dijk katika usajili wa dirisha lijalo la majira ya joto barani Ulaya.

Gazeti la The Sun la Uingereza jana limeeleza kuwa Juventus imemtengea beki huyo donge nono la pauni milioni 150 ambayo ni sawa na Sh bilioni 456.

Miamba hiyo ya serie A inaamini kuwa mholanzi huyo atatafuta changamoto mpya kama timu yake ikibeba ubingwa wa premier msimu huu na wanataka kumfanya awe beki ghali zaidi duniani kwa mara nyingine tena.

banner

Van Dijk ameisaidia Liverpool kutwaa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Kombe la Dunia la Klabu na Uefa Super Cup huku wakiwa mbioni kubeba ubingwa wa kwanza wa Premier baada ya kupita miaka 30 tangu alipotua Anfield.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited