Home Makala Kapombe,Tshabalala Wajifunga Simba sc

Kapombe,Tshabalala Wajifunga Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji Shomari Kapombe na Mohamed Hussein wameongeza mikataba mipya kuendelea kusalia katika klabu ya Simba sc kwa misimu miwili zaidi na kuzima tetesi za kutakiwa na timu za nje ya nchi.

Simba sc imeendelea na maboresho ya kuongeza wachezaji wapya klabuni hapo huku pia ikifanikiwa kuwabakisha mastaa hao ambao wameonyesha viwango vikubwa kwa zaidi ya misimu mitano sasa wakifanikiwa kuwaweka benchi mpaka mastaa wa kigeni wanaokuja klabuni hapo katika nafasi zao.

Simba sc imeendelea kufaidi ubora wa Kapombe tangu imsajili kutokea Azam Fc japo amekua akisumbuliwa na majeraha kadhaa lakini amekua na kiwango kizuri anapokua uwanjani.

banner

Mohamed Hussein tayari alikua na ofa kutoka nchini Afrika ya kusini lakini uimara wa Simba sc kiuchumi msimu huu umekua nguzo kubwa kwa klabu hiyo kumbakisha staa huyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited