Baada ya kocha mkuu wa Mtibwa Sugar,Zuberi Katwila kumwaga manyanga jana Oktoba 18, ndani ya kikosi hicho ambacho alikuwa nacho kwa muda mrefu ameibukia Ihefu Fc ya Mbeya.
Katwila anachukua mikoba ya Maka Mwalwisi aliyefutwa kazi Oktoba 6 ndani ya Ihefu FC kutokana na mwendo mbovu wa timu hiyo ambayo imepanda ligi kuu bara msimu huu 2020/2021.
Akiwa Mtibwa Sugar aliambulia ushindi mchezo mmoja dhidi ya Ihefu FC kwa kuifunga bao 1-0 na alilazimisha sare mbili huku akipoteza mechi tatu katika raundi sita.