Home Makala Kaze Kufungua Dimba Na Polisi Tanzania

Kaze Kufungua Dimba Na Polisi Tanzania

by Sports Leo
0 comments

Cedric Kaze ambaye ni kocha mkuu wa Yanga Sc tayari ameshaanza kazi ya kukinoa kikosi hicho cha Jangwani ambacho Novemba 22,kitavaana na Polisi Tanzania uwanja wa Mkapa.

Kocha huyo aliyesaini kandarasi ya miaka miwili kukipa makali kikosi cha Yanga Sc atakutana na Polisi Tanzania ambayo iko nafasi ya 7 na pointi 10 ikiwa imecheza mechi tano huku kikosi chake kikiwa nafasi ya tatu na pointi 13.

Mchezo huo wa raundi ya sita wa ligi kuu unatarajiwa kuchezwa majira ya 1:00 usiku ambapo kutakuwa na ushindani mkubwa kwani kila timu itakuwa ikisaka pointi tatu muhimu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited