Home Makala Kisa Corona ,Niyonzima Amvuta Kaseja

Kisa Corona ,Niyonzima Amvuta Kaseja

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Yanga Sc ,Haruna Niyonzima amelazimika kuwavuta karibu kwenye mazoezi ya pamoja wakongwe wenzake ,Juma Kaseja na Shabani Kado ikiwa ni mikakati mahususi ya kujiandaa  na tamko la shirikisho la soka Tanzania(TFF)la kurejea kwa ligi kuu Bara.

Awali nyota huyo alikwa akifanya mazoezi mara moja kwa siku nyumbani kwake baada ya ligi kusimamishwa,lakini kwa sasa ameamua kuungana na kaseja pamoja na Kado ambapo wanafanya mazoezi hayo mara mbili kwa siku katika ufukwe wa Escape One ,Mikocheni.

“Nilikuwa nafanya kweli mazoezi mara moja tena nyumbani  maana kuna nafasi ya kutosha ambayo ilikuwa inaniwezesha kwenda na program za kocha,ila kadri siku zinavyoenda  nimelazimika kuongeza muda wa mazoezi ambapo sasa hivi nafanya na Kaseja pamoja na Kado”

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited