Home Makala Kisa Horoya Fc,Mabosi Simba sc Waweka 200m

Kisa Horoya Fc,Mabosi Simba sc Waweka 200m

by Sports Leo
0 comments

Viongozi wa klabu ya Simba wamewaahidi wachezaji kuwapa kitita Cha Shilling milioni 200 kama watapata alama tatu kwenye mchezo wa mzunguko wa Tano wa kundi C katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Horoya,

Ikumbukwe kuwa mchezo huo utapigwa siku ya Jumamosi ya wiki hii katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam majira ya saa Moja kamili usiku ambapo endapo Simba sc itawafungwa Horoya Fc basi itakua na uhakika wa kwenda robo fainali kama mshindi wa pili wa kundi C nyuma ya Raja Casablanca.

Msimamo wa kundi hilo mpaka sasa ni Simba sc wapo nafasi ya pili wakiwa na alama sita huku Raja Casablanca wakiwa kileleni na alama 12 na Horoya Fc wakiwa nafasi ya tatu na alama nne huku Vipers Fc wakishika mkia na endapo Simba sc atafanikiwa kuwafunga basi atafikisha alama tisa ambazo haziwezi kufikiwa na Horoya wala Vipers.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited