Home Makala Kisinda Akwama Yanga sc

Kisinda Akwama Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imekwama katika mpango wake wa kumtumia Tuisila Kisinda katika kikosi cha timu hiyo katika mashindano ya ndani na nje ya nchi baada ya Shirikisho la soka nchini kuzuia usajili wake wakisema tayari klabu hiyo ilishakamilisha usajili wa wachezaji wa kigeni katika mfumo wa usajili wa Fifa.

Yanga sc ilimsajili Kisinda dakika za mwisho huku ikimuondoa Lazarus Kambole katika orodha ya wachezaji wake baada ya kuumia katika mchezo wa kirafiki hivyo kuhitaji muda mrefu zaidi wa matibabu na kuilazimisha klabu kuchukua maamuzi hayo.

Taarifa zilizosambaa hivi leo na kuwa gumzo kwa wadau wa soka nchini ni Shirikisho la soka nchini kuzuia usajili huo kuuingiza katika mfumo huku likigoma kumuondoa Kambole katika usajili huo likisema tayari lilishakamilisha mchakato wa kuwasajili wachezaji wa ndani na nje kwa timu zinazoshiriki michuano ya kimataifa.

banner

Tayari shirikisho hilo la soka nchini limetoa maelekezo juu ya sakata hilo japo bado kwa upande wa Yanga sc mpaka sasa hawajatoa tamko lolote juu ya suala hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited