Kipa wa Yanga Mkenya Farouk Shikalo amefurahishwa na kurejea kwa beki mkongwe Kelvin Yondani ambaye aligoma kujiunga na kambi ya timu hiyo baada ya kutokamilishiwa baadhi ya madai yake ya fedha na klabu hiyo.
Beki huyo amejiunga na kambi hiyo iliyopo mkoani Kilimanjaro ambapo wanajiandaa na mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Fc na Afc Leopard kabla ya kuwavaa Township Rollers nchini Botswana.

Kelvin Yondani
Farouk amefurahishwa na ujio wa beki huyo kutokana na uimara aliokua nao kukabana na washambuliaji wakorofi akikumbuka alivyomkaba Michael Olunga wa kenya wakati timu hizo zilipokutana katika michuano ya Afcon nchini Misri.
“Ni beki mzuri na mzoefu,imenichukua dakika tano tu mazoezi kubaini uimara wake”alisema Shikalo
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Yanga inakabiliwa na mchezo muhimu dhidi ya Rollers baada ya mechi ya awali iliyofanyika jijini kuisha kwa sare ya moja kwa moja.