Premier League msimu huu umeanza vizuri sana baada ya wikiendi iliyopita kuwepo na mtanange wa kukata na shoka,huku jumatatu ya kesho Liverpool watawakaribisha maasimu wao Arsenal katika uwanja wao wa nyumbani Anfield ili kuendelea kunogesha EPL saa 4 usiku.
Mchezo huo wa kesho unakuwa ni wa burudani sana kwa mashabiki kesho kwani si mara ya kwanza kwa timu hizi kukutana msimu huu,kwani tayari Arsenal walishawaburuza Liverpool katika mchezo wa ngao wa jamii.
Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu England wanasubiri kwa hamu kuona kama Arsenal watarudia walichokifanya siku ya ngao ya jamii kwani mechi itakuwa ni ya kisasi ili kila mmoja aweze kuzipata pointi tatu muhimu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.