Home Makala Luís Miquissone Atambulishwa Simba sc

Luís Miquissone Atambulishwa Simba sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba sc imemtambulisha rasmi Luís Miquissone kuwa mchezaji wao mpya baada ya kuondoka klabuni hapo takribani misimu miwili iliyopita na kwenda kujiunga na Al Ahly ya nchini Misri.

Simba sc imemrejesha mchezaji huyo kwa kuamua kumpa mkataba wa miaka mitatu akiwa kama mchezaji huru baada ya kufanikiwa kuvunja mkataba wake na klabu ya Al Ahly kwa makubaliano ya pande mbili.

Luís Miquissone tangu asajiliwe na mabingwa hao wa Afrika amekua akitolewa kwa mkopo mara kadhaa hasa baada ya kukosa namba katika kikosi cha kwanza tangu aondoke kocha Pitso Mosimame ambaye alimsajili.

banner

Mchezaji huyo tayari yupo nchini akishughulikia taratibu za safari ili ajiunge na kambi ya timu hiyo nchini Uturuki kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu na michuano ya kimataifa ambapo Simba sc itashiriki michuano maalumu ya Super League.

Simba sc imekua na misuli ya usajili za gharama msimu huu hasa baada ya kupata takribani bilioni 5 za maandalizi ya michuano hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited