Home Makala Man Utd Aibu Tupu

Man Utd Aibu Tupu

by Sports Leo
0 comments

Ni aibu,ndio neno fupi unaweza kusema kutokana na klabu ya Manchester United kupokea kipogo cha mabao 4-0 kutoka kwa mahasimu wao Liverpool katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza uliofanyika katika uwanja wa Anfield jijini Liverpool.

Iliwachukua Liverpool dakika 5 tu kupata bao la kwanza likifungwa na Luiz Dias kutokana na safu ya ulinzi ya Man united kutokua na maelewano ya kutosha chini ya nahodha Harry Maguire huku Mo salah akifunga bao la pili dakika ya 22 ya mchezo ambapo mpaka mapumziko matokeo yalibaki kuwa hivyo.

Kipindi cha pili kilikua kigumu zaidi kwa Man United kwani waliruhusu mabao mengine mawili kupitia kwa Mo salah na Sadio Mane huku umiliki w mchezo ukiwa ni asilimia 78 kwa Liverpool na 22 kwa Manchester United huku Liverpool wakipiga mashuti 5 golini kwa United ambapo mashuti manne yalizaa mabao huku Man Utd ikipiga shuti moja pekee.

banner

Kutokana na matokeo hayo Liverpool wanasalia kileleni wakiwa na alama 76 huku Man United wakiwa nafasi ya sita na alama 54 katika michezo 33 ya ligi kuu nchini humo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited