Home Makala Man Utd Gari Limewaka

Man Utd Gari Limewaka

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Manchester United imekua na matokeo mazuri mfululizo baada ya kufanikiwa kuwachapa Everton 3-1 katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika katika uwanja wa Old Trafford jijini Manchester ikiwa ni mchezo wa kombe la Fa raundi ya tatu ya michuano hiyo.

Ushindi huo ni wa saba mfululizo katika michuano yote iliyocheza siku za karibuni huku ikionyesha mwendelezo mzuri uwanjani huku mastaa wakijitoa ipasavyo kupambania alama tatu ambapo mapema dakika ya nne Antony aliifungia klabu yake goli la kwanza ambalo lilisawazishwa dakika ya 14 na Conor Coady lakini Conor Goady alijifunga dakika ya 52 huku Rashford akiongeza bao la tatu dakika za mwishoni za nyongeza.

Katika mchezo huo Marcus Rashford alionyesha kiwango kizuri huku akifunga katika michezo mitano mfululizo na kumuweka matatani kocha Frank Lampard ambaye licha ya kikosi chake kupoteza pia hakikua katika fomu nzuri huku mashabiki wa klabu hiyo wakichukizwa na matokeo hayo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited