Home Makala Man Utd Yaibomoa Ajax Fc

Man Utd Yaibomoa Ajax Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Manchester united imefikia makubaliano na Fc Ajax ya kumnunua beki Lisandro Martinez kwa dau linalotajwa kuwa kiasi cha paundi milioni 46 ambapo sasa mchezaji anakamilisha taratibu zingine ndogondogo za usajili ikiwemo kupimwa afya.

Usajili huo unaelekea kukamilika baada ya taarifa za muda mrefu kuhusu uwepo wa dili hili huku kikwazo kilikua ni makubaliano ya dau la usajili ambapo inasemekana mchezaji alikua tayari kwa uhamisho kwenda kuungana na kocha wake wa zamani Erick Ten Hag huku ilifikia hatua akitaka kugoma kufika mazoezini ili kulazimisha dili hilo.

Martinez ataungana na Ericksen ambaye tayari amekamilisha usajili kujiunga na timu hiyo huku akiwatosa vigogo kama Arsenal ambao nao walikua wanamnyemelea staa huyo mwenye uwezo wa kucheza kama beki wa kati na kushoto pamoja na kiungo mkabaji.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited