Klabu ya Manchester united imefikia makubaliano na Fc Ajax ya kumnunua beki Lisandro Martinez kwa dau linalotajwa kuwa kiasi cha paundi milioni 46 ambapo sasa mchezaji anakamilisha taratibu zingine ndogondogo za usajili ikiwemo kupimwa afya.
Usajili huo unaelekea kukamilika baada ya taarifa za muda mrefu kuhusu uwepo wa dili hili huku kikwazo kilikua ni makubaliano ya dau la usajili ambapo inasemekana mchezaji alikua tayari kwa uhamisho kwenda kuungana na kocha wake wa zamani Erick Ten Hag huku ilifikia hatua akitaka kugoma kufika mazoezini ili kulazimisha dili hilo.
Martinez ataungana na Ericksen ambaye tayari amekamilisha usajili kujiunga na timu hiyo huku akiwatosa vigogo kama Arsenal ambao nao walikua wanamnyemelea staa huyo mwenye uwezo wa kucheza kama beki wa kati na kushoto pamoja na kiungo mkabaji.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.