Home Makala Man Utd Yasajili Beki Mapafu ya Mbwa

Man Utd Yasajili Beki Mapafu ya Mbwa

by Dennis Msotwa
0 comments

Manchester United imekamilisha usajili wa beki Aaron Wan-Bissaka kutoka klabu ya Crystal Palace kwa kiasi cha paundi 50m bei ambayo imemfanya beki huyo kuwa beki wa pembeni ghali zaidi kwa sasa.

Wan-Bissaka amesajiliwa baada ya majadiliano ya muda mrefu baina ya timu hizo mbili hasa kuhusu dau la usajili japo mchezaji huyo alishakubaliana na man united mshahara wa paundi elfu 80 kwa wiki.

Beki huyo anayeichezea timu ya vijana ya Uingereza chini ya miaka 21 ni zao la akademia ya timu hiyo na alipandishwa timu ya wakubwa na kufanikiwa kucheza michezo 46 tu iliyomfanya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa klabu hiyo kwa msimu huu wa ligi ulioisha.

banner

Bissaka atatambulishwa rasmi leo hii ijumaa kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu hiyo baada ya kuwa jijini manchester kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kujiunga na klabu hiyo ikiwemo kufanyiwa vipimo vya afya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited