Home Makala Manyika Kufanya Maajabu Polisi

Manyika Kufanya Maajabu Polisi

by Sports Leo
0 comments

Golikipa aliyewahi kuichezea Simba Sc na Singida United Peter Manyika ameaminika mbele ya uongozi wa Polisi Tanzania kuwa atafanya vizuri katika mechi za ligi kuu bara na mashindano ya kombe la FA.

Polisi Tanzania inayomilikiwa na jeshi la polisi nchini ilimsajili Manyika katika usajili wa dirisha dogo mwezi huu akitokea katika klabu ya KCB inayoshiriki ligi kuu Kenya.

Munisi alisema kuwa wanaamini kuwa Manyika ni mmoja wa watakaowavusha katika msimu huu ili kufikia nafasi ya tatu za juu na waweze kucheza fainali za kombe  la FA linalotoa tiketi za kuwakilisha Tanzania Bara kushiriki kombe la shirikisho Afrika.

banner

Polisi Tanzania ipo nafasi ya 9 katika msimamo wa ligi kuu bara ikiwa imecheza mechi 16 na pointi 24 wakati mabingwa watetezi Simba Sc ina pointi 41 na inaongoza katika msimamo wa ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited