Home Makala Marumo Wawasili Alfajiri

Marumo Wawasili Alfajiri

by Dennis Msotwa
0 comments

Baada ya danadana kuhusu lini watawasili nchini hatimaye msafara wa timu ya Marumo Gallant ya nchini Afrika kusini umefanikiwa kuwasili nchini alfajiri ya leo katika uwanja wa Mwl.Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Mara baada ya kuwasili msafara wa timu hiyo uligomea kupanda basi la lililoandaliwa na wenyeji wao Yanga sc na kupanda basi jingine ambalo wamelitafuta wenyewe na kuelekea hotelini moja kwa moja.

Timu hizo zitakutana kesho katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la shirikisho unaotarajiwa kuanza majira ya saa kumi za jioni katika uwanja wa Benjamini Mkapa ambapo watarudiana tarehe 17 Mei mwaka huu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited