Mastaa wa kikosi cha Azam Fc tayari wameingia kambini kwa ajili ya kuanza mazoezi ya msimu mpya wa 2023/2024 katika uwanja wa Azam Complex Chamazi ambapo watakaa kwa siku mbili kabla ya kwenda visiwani Zanzibar kwa kambi ya siku saba kisha kwenda nchini Morocco.
Timu hiyo inatarajiwa kukaa nchini Morocco kwa takribani wiki mbili kisha itarejea nchini ikiwa na kikosi kilicho tayari kwa ajili ya kuanza michuano ya ngao ya Jamii na kisha kuanza kampeni ya kunyakua taji la ligi kuu ya Nbc nchini Tanzania pamoja na ile ya michuano ya kimataifa ambapo timu hiyo itashiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika.
Katika mazoezi hayo yanayofanyika asubuhi na jioni mastaa wa kikosi hicho wakiwemo Wacolombia waliosajili msimu huu Ever Meza na Jhonier Blanco pamoja na Muivory Coast Franck Tiesse sambamba na beki Mali Yoro Mamadou Diaby wote kwa pamoja wamehudhuria mazoezi hayo.
Pia kipa Ali Ahmada naye ameungana na mastaa wa kikosi hicho baada ya kupona majeraha yake yalimfanya akafanyiwa upasuaji na kukaa nje msimu nusu msimu mzima wa ligi kuu kuanzia mwezi Januari mwaka huu na kumpisha Mohamed Mustafa aliyesajili kwa mkopo kutoka El-Merrikh ya nchini Sudan kabla ya kusajili moja kwa moja dirisha hili.