Home Makala Mastaa Tisa Yanga sc Kuikosa Biashara

Mastaa Tisa Yanga sc Kuikosa Biashara

by Sports Leo
0 comments

Wakati kikosi cha Yanga sc kikitarajiwa kuingia uwanjani muda mfupi ujao imebainika mastaa tisa wataukosa mchezo huo wa hatua ya 16 ya kombe la shirikisho la Azam Sports utaofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Orodha ya mastaa hao Djuma Shabani na Dickson Job ambao wanatumikia adhabu ya kufungiwa huku Djuma akitarajiwa kuwepo mchezo ujao dhidi ya Mtibwa Sugar na Job ndo anaanza adhabu ya mechi tatu kwa kumkanyaga Richarlson Ng’ondya wa Mbeya City wakati walipokutana katika mchezo wa ligi kuu.

Mastaa kama Chico Ushindi,Yassin Mustapha,David Bryson,Kibwana Shomari,Abdala Shaibu,Salum Abubakary,Chrispin Ngushi wenyewe wanasumbuliwa na majeraha mbalimbali huku Yacouba Sogne akiwa amerejea tayari baada ya kuwa nje kwa miezi mitatu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited