Home Makala Matola Atua Simba

Matola Atua Simba

by Sports Leo
0 comments

Kocha Selemani Matola ameanza rasmi kazi ya kuifundisha timu ya Simba akiwa kama kocha msaidizi akitokea Polisi Tanzania baada ya kuvunja mkataba na timu hiyo.

Matola aliyewahi kuwa kocha msaidizi klabuni hapo miaka ya nyuma tayari ameanza kazi hiyo akichukua nafasi ya Dennis Kitambi ambaye amesitishiwa mkataba na klabu hiyo ambayo imeamua kuvunja benchi lote la ufundi lililokua likiongozwa na Patrick Aussems.

Taarifa rasmi iliyotolewa na waandishi wa habari imeonyesha pia kuwa matola atakua kocha mkuu wa timu ya vijana ya timu hiyo kama ambavyo taarifa inavyosomeka.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited