Home Makala Mawaziri Wawili Ndani Ya Kili Marathon

Mawaziri Wawili Ndani Ya Kili Marathon

by Sports Leo
0 comments

Miongoni mwa vigogo wa serikali watakaokimbia kwenye mashindano ya mbio za Kili Marathon ni waziri wa mali asili na utalii Dk.Hamisi Kigwangala na waziri wa habari ,sanaa,utamaduni na Michezo Dk.Harrison Mwakyembe.

Mbio hizo ambazo zimedhaminiwa na kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro Premium Lager zinatarajiwa kufanyika keshokutwa Jumapili zikianzia viwanja vya ushirika mjini Moshi.

John Bayo ambaye ni mjumbe wa kamati ya mbio amesema kuwa waziri Kigwangala ndiye atakayekuwa mgeni rasmi na mwenyeji wake akiwa Dk. Mwakyembe.

banner

Kwa upande wa maandalizi upo hatua ya mwisho ambapo usajili utafungwa kesho saa 6:00 mchana na askari 310 tayari wameshaandaliwa kwa ajili ya kuimarisha usalama barabarani wakati wa mbio hizo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited