Home Makala Makata,Naftari Jela miaka 5

Makata,Naftari Jela miaka 5

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa klabu ya Mbeya kwanza Mbwana Makata na meneja wa klabu hiyo David Naftari wamefungiwa kujihusisha na soka kwa miaka mitano kufuatia kuwashawishi wachezaji kugomea mchezo dhidi ya Namungo ambao ulipangwa kufanyika mkoani Lindi katika uwanja wa Ilulu.

Katika mchezo huo gari la wagonjwa lilichelewa kwa dakika 24 ambapo ilitakiwa mchezo uanze baada ya gari hilo kufika kwa mujibu wa kanuni za ligi kuu ambapo mchezo unaweza usiendelee endapo gari la wagonjwa litachelewa kwa nusu saa hivyo kamati iliwakuta wahusika na kosa la kukiuka kanuni ya 32:7 ya ligi kuu kuhusu kuvuruga mchezo.

Licha ya viongozi hao kufungiwa miaka mitano pia klabu ya Mbeya kwanza imepoteza mchezo huo ambapo Namungo Fc wamepewa alama tatu na magoli matatu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited