Home Makala Mayele Apiga 3 Yanga sc ikiilaza Zalan Fc

Mayele Apiga 3 Yanga sc ikiilaza Zalan Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji Fiston Kalala Mayele amefunga mabao matatu katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Zalan Fc katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika mchezo uliokua wa upande mmoja uliofanyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.

Licha ya kuongoza kwa umiliki wa mpira kipindi chote cha mchezo iliwalazimu Yanga sc kusubiri mpaka dakika ya 49 ya kipindi cha pili ili kupata bao la uongozi lililofungwa na Fiston Kalala Mayele ambae aliunganisha kwa kichwa krosi ya Dennis Nkane aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Dickson Ambundo ambaye alianza kipindi cha kwanza.

Dakika tano baadae Feisal Salum alipokea pasi ya Jesus Moloko na kuwachambua mabeki wa Zalan Fc na kuandika bao la pili lililoamsha furaha ya mashabiki wa Yanga sc huku Fiston Mayele akifunga bao la tatu na nne dakika ya 84 na 87 na kuwalazimisha waamuzi kumpa mpira baada ya kufunga mabao matatu katika mchezo mmoja kama ulivyo utaratibu wa siku zote.

banner

Klabu hizo zinatarajiwa kurudiana wiki ijayo ambapo Yanga sc itakua mwenyeji wa mchezo huo ambao utafanyika katika uwanja huo huo baada ya Zalan Fc ya nchini Sudan kusini kutokua na uwanja nchini mwao ambao umeidhinishwa na Caf hivyo kuwalazimu kuutumia uwanja wa Benjamin Mkapa kama uwanja wa nyumbani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited