Home Makala Mbaraka Arudi Nyumbani Kagera Sugar

Mbaraka Arudi Nyumbani Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji wa Azam Fc,Mbaraka Yusuph amesaini kandarasi ya miaka miwili kuichezea timu yake ya zamani ya Kagera Sugar baada ya mkataba wake kumalizika ndani ya Azam.

Mbaraka alisajiliwa hapo awali na Azam Fc akitokea Kagera Sugar baada ya kuwa mfungaji bora ila kwa sasa anarejea nyumbani Bukoba kutokana na kutokuwa na msimu mzuri ndani ya kikosi hicho kwa takribani miaka mitatu huku akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara.

Baada ya kusaini mkataba huo Mbaraka amesema kuwa ni wakati wake wa kurejea nyumbani na yupo tayari kuucheza mpira haswa kwani ni mchezaji huru kwa sasa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited