Wakati Bernard Morrison mchezaji wa Yanga akiendelea kuwafanya wapenzi wa timu hiyo washindwe kuamini anachofanya uwanjani baada ya kuhaidi kuifanyia maajabu timu hiyo Luc Eymael ambaye ni kocha mkuu wa Yanga ameshusha kifaa kingine jijini kimyakimya raia wa Ghana, Joseph Quansah.
Quansah mwenye umri wa miaka 29 ametokea katika klabu ya Amodaus Professional na tayari ameshamwaga wino kuichezea Yanga miaka miwili ana uwezo katika dimba la kati huku akiwa na vionjo kama vya mtangulizi wake Morrison.
Habari njema kwa Wanayanga ni kuwa kocha wao Eymael ameahidi kukamilisha idadi yake kwa kushusha mchezaji mwingine ili kufikisha idadi ya watatu anaowahitaji kikosini na anajua sehemu atakayowatoa wachezaji hao kwa kuwaalishindwa kuwasajili dirisha dogo baada ya kuchelewa kutua nchini.