Home Makala Mbeya City Atupia Mabao 2-1 Leo

Mbeya City Atupia Mabao 2-1 Leo

by Sports Leo
0 comments

Mbeya City imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa leo Octoba 23,wa ligi kuu bara uliochezwa uwanja wa Kaitaba.

Kwa mara ya kwanza Mbeya City leo wanasepa na pointi tatu kwa msimu wa 2020/21 tangu kuanza wa ligi ikiwa ni raundi ya nane.

Mabao ya Mbeya City yalifungwa na Abdurazack Mohamed  kwa mkwaju wa penalti dakika ya pili huku lile la pili lilifungwa dakika ya 24 na Siraj Juma.

banner

Bao la kufutia machozi la Kagera Sugar lilipachikwa kupitia Erick Kyaruzi dakika ya 46.

Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City kutoka nafasi ya 18 iliyokuwa kwa muda wa raundi saba na sasa ipo nafasi ya 16 ikiwa na pointi tano baada ya kucheza mechi nane ndani ya ligi huku Kagera Sugar inabaki nafasi ya 15 ikiwa imecheza mechi nane na pointi tano zikiwa zimetofautiana kwenye mabao ya kufungwa na kufungana.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited