Home Makala Mbrazil Atua Singida FG

Mbrazil Atua Singida FG

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Singida Big Stars imemtambulisha rasmi kocha wao mpya Ricardo Ferreira kutoka nchini Brazil ambaye anakuja kuchukua nafasi ya kocha Enrst Middendorp ambaye aliamua kujiuzuru ghafla kuifundisha timu hiyo.

Kocha Ricardo ana rekodi ya kufundisha vilabu vikubwa barani Afrika kwa mafanikio vikiwemo Al Hilal, Al Merrikh SC na Ismaily SC hivyo anatarajiwa kutoa upinzani mkubwa kwa klabu zinazokutana na timu hiyo hasa katika ligi kuu nchini.

Kocha huyo amesaini kandarasi ya mwaka mmoja kuinoa timu hiyo ambapo anatarajiwa kuchukua nafasi ya Mathias Lule na Thabo Senong waliokuwa wanaiongoza baada ya kuondoka kwa kocha mkuu Ernst Middendorp.

banner

Tayari timu hiyo iliamuajiri kocha Peter Manyika kuja kuwanoa makipa wa klabu hiyo huku ikitajwa kuwa kocha Zubeiry Katwila pia anakuja kuungana nae kama kocha msaidizi wa klabu hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited