Home Masumbwi Mdomo Wamponza Wilder

Mdomo Wamponza Wilder

by Sports Leo
0 comments

Bondia Tyson Furry amefanikiwa kumpiga bondia Deontay Wilder na kuchukua ubingwa wa dunia wa uzito wa juu katika pambano lililofanyika leo Las Vegas Marekani.

Pambano hilo lililotikisa dunia katika mizani ya uzito wa juu ambapo Furry alikua anasaka heshima baada ya kuhisi alidhulumiwa ushindi katika pambano la awali disemba mwaka 2018.

Furry alifanikiwa kumuangusha Wilder mapema raundi ya tatu tu licha ya bondia huyo kuanza kwa kasi na mpaka kufika raundi ya tano tayari Furry alianza kunusa ushindi baada ya kumuangusha tena Mmarekani huyo.

banner

Pambano lilimalizika raundi ya saba baada ya timu ya Wilder kurusha taulo uwanjani kiashiria cha kukubali pambano liishe ili kumuokoa bondia wao baada ya kumuona amezidiwa na makonde.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited