Mabosi wa klabu ya Simba sc wana mpango wa kumhamishia kocha Juma Mgunda kuwa kocha mkuu wa klabu ya Simba queens ili kupisha nafasi ya kocha Roberto Oliveira kuja na kocha msaidizi ambaye anamtaka ili kupata uhakika wa kuleta makombe zaidi klabuni hapo.
Robertinho amewaomba mabosi wa klabu hiyo aje na wasaidizi wake akianza kuja na kocha wa viungo kutoka Rwanda Hategekimana Corneille na sasa analeta msaidizi wake hivyo kuwalazimu mabosi wa klabu hiyo kufanya maamuzi hayo mazito ya kufyeka benchi la ufundi wakianza kuwaondoa Seleman Matola na Patrick Rweyemamu.
Pia kumekua na tetesi za kocha huyo kutaka kurejea Coastal Union ambapo amezakanusha kabisa huku akisema kuwa bado ana mkataba na Simba sc.
“Mmefanya vizuri kuniuliza, kwani majibu yangu yatawapa kujua bado ni mfanyakazi wa Simba. Kuhusu Coastal siwezi kukataa kwamba ni timu yangu ambayo nimetoka nayo mbali, tukirekebisha matatizo yetu tutaendelea salama,” alisema kocha huyo ambaye amejiwekea rekodi nzuri Simba.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Nipo Tanga kwa mapumziko utakapofika muda wa kurejea kwenye majukumu Simba mashabiki wangu wataniona,”alisema na kuongeza kuwa msimu uliomalizika aliuona ushindani mkubwa ambao unawapa picha ya kufanya maandalizi makubwa zaidi kwa ajili ya ujao.
“Ligi ina ushindani mkali na soka linakuwa, hivyo kila timu itakuwa inajipanga kulingana na mahitaji yake ya msimu mwingine,” alisema Mgunda