Home Soka Mgunda Atwaa Tuzo Mei

Mgunda Atwaa Tuzo Mei

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha wa klabu ya Simba sc Juma Mgunda ametwaa tuzo ya Kocha bora  wa mwezi Mei baada ya kuwashinda Kocha wa Yanga sc Miguel Gamondi na kocha wa Azam Fc Bruno Ferry ambapo kocha ameifanya klabu yake kuvuna alama nyingi zaidi kwa mwezi huo.

Mgunda alivuna jumla ya alama 19 katika michezo saba aliyocheza klabu yake ya Simba sc ikivuna alama tatu katika michezo sita huku ikipata sare katika mchezo mmoja na kuifanya klabu hiyo kumaliza ligi kuu katika nafasi ya tatu na kukata tiketi ya michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.

Kati mechi hizo sita ambazo Simba sc ilishinda imo ambayo aliiongoza kuifunga Azm Fc kwa mabao 3-0 katika uwanja wa Benjamin Mkapa kinyume na matarajio ya wengi kuwa Simba sc ingepoteza mchezo ule kwa idadi kubwa ya mabao kutokana na kutokua na kiwango kizuri huku ikiwakosa mastaa kibao kikosini.

banner

Mgunda amekua akitumika klabuni hapo kama kocha wa muda baada ya makocha wakuu kutimuliwa mara kwa mara hali iliyozua maswali kuhusu hatma yake klabuni hapo ambapo alijiunga akitokea Coastal Union japo amekua na mchango mkubwa akishika timu kama kocha mkuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited