Home Makala Mmiliki Wa Ihefa Fc Afariki

Mmiliki Wa Ihefa Fc Afariki

by Sports Leo
0 comments

Ihefa fc Imepata pigo kubwa baada ya kupokea taarifa za kifo cha aliyekuwa mmoja wa wamiliki wa timu hiyo,Abdulhaq Pirmohamed.

Mmiliki huyo alianza kuugua siku kadhaa kabla ya umauti kumkuta siku ya jana Alhamisi,wakati alipofanyiwa upasuaji aligundulika kuwa na mawe kwenye figo.

Wakati wakimfanyia upasuaji mgonjwa alipata mshtuko wa moyo ambapo ilibidi madaktari kutumia njia mbadala kumsaidia kupumua,lakini licha ya juhudi zote kufanyika hali ilibadilika jana ghafla na akaaga dunia alfajili ya jana na kuzikwa siku hiyohiyo kwenye makaburi ya kisutu,Dar-es-Saalam.

banner

Ihefa Fc ligi daraja la kwanza (FDL) inashika nafasi ya pili kundi A kwa pointi 39 sawa na Dodoma inayoongoza msimamo kwa uwiano mzuri wa mabao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited