Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Simba Sc,Mohammed Dewji ambaye pia ni mwekezaji wa simba amewaambia wekundu hao wa msimbazi wajipange kwa ajili ya kombe la shirikisho la Azam (ASFC) linalotarajiwa kufanyika Agosti 2,mkoani Sumbawanga katika uwanja wa kumbukumbu wa Nelson Mandela.
Mwekezaji huyo amewatia moyo Simba baada ya jana kupoteza alama tatu mbele ya Mbao Fc kwa kipigo cha mabao 3-2 na anaamini kuwa wanaweza kutwaa ubingwa wa ASFC.
“Tusonge mbele tujipange kwa ajili ya fainali ya kombe la shirikisho ASFC) Agosti2,2020.Simba Nguvu Moja”alisema Dewji