Home Makala Morrison Kutua Kengold Fc

Morrison Kutua Kengold Fc

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa zamani wa klabu za Simba Sc na Yanga Sc Bernard Morrison yupo mbioni kujiunga na Klabu ya Kengold Fc yenye makazi yake Wilayani Chunya Jijini Mbeya.

Nyota huyo raia wa Ghana anajiunga na miamba hiyo ya Mbeya kwa mkataba wa miezi 6 kama mchezaji huru ukiwa ni moja ya mikakati ya mabosi wa klabu hiyo kuiepusha kushuka daraja.

Lengo la kumsajili staa huyo ni kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo inayoshika mkia katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini.

banner

Kocha mkuu wa Kengold Fc Omary Kapilima ameonekana kuvutiwa na staa huyo huku akijipanga kumdhibiti upande wa nidhamu ambapo mchezaji huyo amekua na matukio mengi nje ya uwanja ambayo huathiri kiwango chake mara nyingi.

Mbali na Morrison mabosi hao wanaangalia uwezekano wa kusajili mastaa wengine wenye uzoefu akiwemo Obrey Chirwa na Kelvin Yondani.

Katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini klabu hiyo mpaka sasa ipo katika nafasi ya mwisho ikiwa na alama sita pekee katika michezo 16 ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited