Unamkumbuka mshambuliaji wa zamani wa Simba sc na Kagera sugar?ambaye alitamba kisha akasajiliwa Azam fc?
Baada ya kuwa nje ya dimba takribani mwaka mmoja akiuguza majeraha ya goti, mshambuliaji wa azam fc Mbaraka Yusuph, amejumuika na wenzake mazoezini leo Jumapili baada ya kupona majeraha ya goti.
Yusuph alifanyiwa upasuaji wa goti lake la mguu wa kulia Aprili mwaka jana katika Hospitali ya Vincent Pallotti jijini Cape Town, Afrika Kusini, kufuatia kubainika kuchanika mtulinga wa kati wa goti hilo (Anterior Cruciate Ligament Tear).
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Licha ya kusahaulika kutokana na majeraha bado Mbaraka sio mshambuliaji wa kubeza hasa anapokua na utimamu wa mwili.