Home Makala Mtasingwa Ajifunga Azam Fc

Mtasingwa Ajifunga Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imefanikiwa kumuongezea mkataba mpya wa miaka miwili kusalia klabuni hapo kiungo wake Adolph Mtasingwa Bitegeko ambaye alikua anamaliza mkataba wake Januari mwakani.

Awali tetesi zilisema kuwa kiungo huyo alishamalizana na klabu ya Yanga sc kwa kukubaliana kila kitu ambapo ilikua ikisubiriwa amalize mkataba wake ili atue jangwani.

Leo mapema klabu hiyo ya Azam Fc imethibitisha kumuongezea mkataba mpya ambapo atadumu klabuni hapo mpaka mwaka 2027 huku usajili huo ukimfurahisha kocha Yousouph Dabo wa klabu hiyo kutokana na bado alikua na mahitaji na kiungo huyo.

banner

Mtasingwa alikulia katika akademia ya Azam Fc kisha mwaka 2019 alijiunga na KR Reykjavik ya nchini Iceland na baadae alijiunga na klabu ya Koflavik kisha akarejea KR Reykjavik kisha akajiunga na Volsungur na baadae alirejea Azam Fc msimu wa 2023 mwezi January.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited