Home Makala Mtibwa Sugar Watimua Kocha

Mtibwa Sugar Watimua Kocha

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klab ya Mtibwa sugar umefikia maamuzi ya kuachana na Aliyekuwa kocha wao Mkuu Habib kondo baada ya kuwa na mwenendo usio ridhisha kikosini humo hasa katika michuano ya ligi kuu nchini.

Mpaka sasa timu hiyo katika michezo mitano ya ligi kuu haijafanikiwa kuibuka na ushindi wowote ambapo imepata sare mbili huku ikipoteza michezo mitatu na kuifanya iwe katika hatari ya kushuka daraja mkiani mwa msimamo wa ligi kuu.

Kutokana na kutimuliwa kwa kocha huyo sasa timu hiyo itakua chini ya kocha msaidizi Awadh Juma mpaka pale kocha mkuu atakapopatikana huku kukiwa na tetesi za kurejeshwa kwa kocha Zubeiry Katwila ambaye wiki iliyopita alijiuzuru kuifundisha timu ya Ihefu Fc.

banner

Katwila alikua kocha wa zamani wa Mtibwa Sugar mpaka alipoamua kuachia ngazi na kujiungana na Ihefu Fc msimu wa 2021 na sasa anatajwa kurejea klabuni hapo ambapo pia anahusishwa na kujiunga na Singida Fountain Gate Fc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited