Home Makala Mtibwa Waboresha Benchi La Ufundi

Mtibwa Waboresha Benchi La Ufundi

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa Mtibwa Sugar umefanya maboresho katika benchi lake la ufundi leo Agosti 28,kwa ajili ya msimu wa 2020/2021 unaotarajiwa kuanza Septemba 6.

Mabosi hao wamemteua Zubery Rashid Katwila kuendelea kukiongozi kikosi cha Mtibwa Sugar kama kocha mkuu akisaidiana na Vicent Barnabas ambaye awali alikuwa kocha mkuu wa timu ya Vijana.

Mtibwa Sugar imefanya pia mabadiliko katika nafasi ya kocha wa makipa kwa kumtambulisha Soudy Slim aliyewahi kuwa mchezaji wa Mtibwa sugar huku daktari wa timu akiwa ni Lawrance Mushi.

banner

Wengine ni Amir Abdallah ambaye ameteuliwa kuwa msimamizi wa vifaa vya timu na meneja wa timu ni David Chitty B’-goya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited