Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza majina sita ya waamuzi watakaochezesha mchezo wa fainali kombe la Azam (ASFC) utakaofanyika Jumapili August 2,2020 mkoani Sumbawanga Uwanja wa Nelson Mandela kati ya Simba Sc na Namungo Fc.
Abubakari Mturo kutoka Mtwara ni moja ya muamuzi atakayekuwepo katika mchezo huo baada ya kutoka kwenye kifungo cha miezi mitatu tangu Februari baada ya kushindwa kumudu mchezo kati ya Yanga Sc dhidi ya Lipuli Fc.
Waamuzi wengine wakiwa ni Abdallah Mwinyimkuu kutoka Singida,Ahmed Arajiga kutoka Manyara,Ramadhani kayoko kutoka Dar-es-salaam,Abdullaziz Ally kutoka Arusha na Hamdan Said kutoka Mtwara.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.