Klabu ya Yanga sc imemtambulisha kiungo wao mpya raia wa Ivory Coast Pacome Zouazoua ambaye amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili kuja kusaidia mwendelezo wa kunyakua makombe klabuni hapo.
Kiungo huyo mshambuliaji ndie mchezaji bora wa ligi kuu ya soka ya Ivory Coast akiitumikia klabu ya Asec Mimosas ambapo alifunga mabao saba na kusaidia upatikanaji wa mabao mengine manne katika ligi kuu ya nchini humo.
Pacome anaungana na Stephane Aziz Ki na Koausi Yao ambao wametokea pamoja katika klabu hiyo ya Asec Mimosas ya nchini humo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Kiungo huyo ana uwezo wa kucheza vyema nafasi ya kiungo mshambuliaji na mkabaji ambapo kusajiliwa kwake kunatajwa kuwa anachukua nafasi ya kiungo Yannick Bangala ambaye nae tayari yupo katika harakati za kuondoka klabuni hapo.