Home Makala Mwanuke Awagomea Mabosi Simba sc

Mwanuke Awagomea Mabosi Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Winga Jimmyson Mwinuke amegoma kutolewa kwa mkopo na uongozi wa klabu hiyo kwenda klabu nyingine akishinikiza abaki kikosini ama wavunje mkataba kwa makaubaliano ya pande mbili ili akatafute maisha katika klabu zingine.

Winga huyo ni mmoja katika ya wachezaji ambao uongozi wa klabu hiyo upo mbioni kuwatoa kwa mkopo ili wakaboreshe viwango vyao baada ya kushindwa kumvutia mwalimu Roberto Oliveira “Robertinho”.

Bado haijafahamika sasa kutokana na winga huyo kugoma pendekezo hilo la awali la uongozi juu ya hatma yake klabuni hapo kama watakubali kumuacha moja kwa moja ama ataendelea kubaki kikosini.

banner

Mwanuke alisajili na Simba sc misimu mitatu iliyopita akitokea klabu ya Gwambina Fc iliyokua na makazi yake kanda ya ziwa lakini tangu atue klabuni hapo amekua na nafasi finyu ya kucheza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited